DARAJA MTO MALAGARASI LAKAMILIKA




WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, amesema kuwa ujenzi wa daraja katika Mto Malagarasi, mkoani Kigoma umekamilika.

Dk. Magufuli alitoa kauli hiyo baada ya kufanya ziara katika eneo hilo wiki iliyopita ambapo alisema kuwa ameridhishwa na hatua ya ujenzi huo ulipofikia kwa kiwango cha juu.

“Nimeridhishwa na utendaji wa mkandarasi huyu, hasa kwa jinsi alivyoweza kumaliza sehemu hii ya kwanza kwa muda mzuri na viwango vya hali ya juu,” alibainisha Magufuli.

Alisema Kampuni ya M/S Hanil Engineering and Construction Company Limited za nchini Korea Kusini ziliingia mkataba na kuanza ujenzi wa daraja hilo Desemba 2010 huku wakitakiwa kukamilisha kazi hiyo ifikapo Desemba 2013.

Alisema kuwa mradi huo unajumuisha ujenzi wa madaraja matatu yenye jumla ya urefu wa meta 275  pamoja na barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 48 kwa gharama ya sh bilioni 90 zilizotolewa na Benki ya Exim ya Korea Kusini kwa asilimia 90 huku kiasi kilichobaki kikiwa ni fedha za ndani.

Alisema kuwa hivi sasa kuna ongezeko kubwa la magari kati ya Manyoni – Itingi – Tabora hadi Kigoma kupitia katika Daraja hilo la Kikwete, hali ambayo awali ililazimu kupitia barabara ya Manyoni – Singida - Nzega – Kahama – Nyakanazi – Kibondo – Kasulu hadi Kigoma.

Naye Mhandisi wa mradi huo, Yu Sing, wa Kampuni ya Hanil Engineering alisema kuwa mradi huo umegawanywa katika sehemu  mbili.


“Sehemu ya kwanza ambayo ndiyo iliyokamilika ni ujenzi wa madaraja matatu yenye urefu wa meta 25, meta 200 na meta 50 pamoja na kilometa 11 za lami na sehemu ya pili ni ujenzi wa kilometa 37 za lami ambazo zinaendelea kukamilishwa kwa sasa,” alisema.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment