MOTO ULIVYOTEKETEZA MAGHALA YA KIWANDA CHA NYUZI TABORA

 

Maghala mawili ya kuhifadhia nyuzi yaliyopo katika kiwanda cha nyuzi mjini Tabora kinachomilikiwa na mwekezaji mwenya asili ya kiasia, yameteketea kwa moto tangu saa 7 mchana na kusababisha hasara kubwa ambayo haikujulikana mara moja.

Mkuu wa kikosi cha zimamoto manispaa ya Tabora Bw. Farijara amesema kuwa katika harakati za kuzima moto huo usisababishe madhara sehemu ya uzalishaji, moto huo haukuleta madhara kwa binadamu na chanzo bado hakijajulikana.

Mmiliki wa kiwanda hicho amesema kuwa hasara iliyojitokeza katika sehemu hiyo ni kubwa, lakini haitaathiri sehemu ya uzalishaji kutokana kuwa na malighafi sehemu nyingineambazo hazijateketea kwani sehemu iliyoteketea ni sehemu ya mali ambayo ilikuwa imesindikwa tayari.


Hata hivyo watumishi wa kiwanda hicho wamemshukuru Mungu kutokana na moto huo kuwaka wao wakiwa mapumziko ya chakula, kwani ingeweza kuleta madhara kwa maisha ya watu ambao hufanya kazi ndani ya maghala hayo,  huku wakisikitikia hasara iliyojitokeza kwani ni sehemu ya uzalishaji wa kiwandani hapo.







CHANZO: ITV
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment