MATATIZO YATOKANAYO NA UBEBAJI WA TEMBE ZA MADAWA YA KULEVYA KWA NJIA YA UTUMBO

 Na Rajab Ganga


Ni hatari kubwa kutumia kubeba madawa ya kulevya kwa njia ya tumbo njia hii imewaathiri wengi ambao matokeo yake ni:

KIFO

Kifo hutokea kwa mbebaji wa madawa kwa njia ya utumbo ambae humeza madawa haya ili kujizuzia na kukamtwa na vikosi vya usalama wakitumia njia hiyo kuwa ni salama matokeo yake ni uzito kumzidi mbebaji na baadhi ya tembe kuingia katika njia ya nje ya utumbo ikipelekea kupasuka kwa tembe hizo wanasema kurishai.

MATATIZO YA TUMBO

mbebaji wa madawa tumbo lake mara kwa mara huhisi maumivu kutokana na ugumu wa tembe hizo zinapozama tumboni kwa muda mrefu na kipindi kirefu, tembe hizo husongamana na kuta za utumbo na kusababisha maumivu.

KULEGEA KWA NJIA YA HAJA KUBWA

Kitendo cha kutoa madawa kwa njia ya haja kubwa hupelekea mbebaji kulegea sehemu zake za haja kubwa na matokeo yake mfumo wa usafishaji wa haja kubwa hudhoofika na kusababisha maradhi ya fangasi, Cancer na ugonjwa wa kushuka nyama ya haja kubwa maarufu Puru, hayo ni baadhi ya matatizo makubwa yatokanayo na ubebaji wa tembe za madawa ya kulevya kwa njia ya utumbo.

Hizi ni picha za kijana aliefariki akiwa ndani ya ndege akiwa na madawa tumboni na kufanyiwa upasuaji.















Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment