KLABU YA AFRICAN SPORTS YASAKA WADHAMINI


 


Na Rajabu Ganga

UONGOZI wa klabu ya soka ya African Sports ya jijini Tanga umeomba wadau wa mchezo huo kujitokeza katika Kuidhamini klabu hiyo ambayo inakabiliwa na hali ngumu kiuchumi na kupelekea kushindwa kukata kiu ya mashabiki ya kufikia malengo ya kushiriki ligi kuu Tanzania bara.

Msemaji wa klabu hiyo kongwe Said Karisandasi akizungumza kilabuni hapo barabara ya 12 jijini Tanga alisema kuwa klabu hiyo kwa sasa inakabiliwa na uhaba mkubwa wa fedha za kuwezesha shughuli mbali mbali kilabuni hapo.

Karisandas alisema timu  hiyo ambayo kwa sasa inashiriki ligi ya ngazi ya mkoa ikiwania ubingwa huo utakaoiwezesha kushiriki ligi daraja la kwanza msimu ujao imekuwa na tatizo la fedha katika kukidhi mahitaji ya kambi ya wachezaji pamoja na vifaa vya mazoezi.

Aidha Karisandas alisema klabu hiyo inakaribisha makampuni, mashirika mbali mbali pamoja na mdau mmoja mmoja kujitolea kudhamini fedha taslimu na vifaa vya michezo.

Msimu uliopita klabu ya African Sports ilifanikiwa kuibuka na ubingwa wa mkoa wa Tanga baada ya kutembeza  kichapo kikali kwa timu pinzani na hatimaye kumaliza ligi  hiyo ikiweka kibindoni alama 54 za ushindi ikifuatiwa na klabu ya Small Prison ya Maweni Tanga.


African Sports, maarufu kama Wana kimanumanu,  ambao 1988-1989 ilifanikiwa kuchukua ubingwa wa kombe la jamhuri Tanzania ipo mbioni kuhakikisha inarudi katika ushiriki wa ligi kuu Tanzania bara baada ya kupoteza nafasi hiyo msimu wa mwaka 1991-1992.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment