BINTI ABAKWA NA KISHA KUCHOMWA MOTO


Indians participate in a protest against violence against women. (File photo)


GENGE la wanaume watatu nchini India limembaka binti wa miaka 13 na kisha kumuua kwa kumchoma moto katika muendelezo wa matukio ya ubakaji na mauaji katika nchi hiyo ya Kusini mwa bara la Asia.

Jana Jumatano, vyombo vya habari nchini India viliripoti kuwa tukio hilo lilitokea siku ya Jumanne katika Wilaya ya Sirsa Kalaar katika mji wa  Orai katika jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh.

Wanaume hao walimshambulia binti huyo wakati akienda shamba pamoja na dada yake mkubwa.

Baba wa binti huyo anasema kuwa mabinti hao “walipowaambia wabakaji kuwa wataripoti tukio hilo katika kituo cha polisi, walimchoma moto na kukimbia.”

Kwa mujibu wa ripoti hizo, dada wa binti huyo alikimbia kwenda kuomba msaada, lakini aliporejea alimkuta mdogo wake akiugulia maumivu yaliyotokana na moto uliotishia kuyakatisha maisha yake.

Alipoteza maisha akiwa hospitali baada ya asilimia 80 ya mwili wake kuungua vibaya sana, liliripoti gazeti la Times of India la nchini humo.

Kwa sasa Polisi wanamtafuta mwanaume aliyetambuliwa kwa jina la Ram Bahadur na washukiwa wengine wawili wa tukio hilo la kinyama.

Visa vya ubakaji na vifo vinavyotokana na matukio hayo vinaonekana sio tu kuongezeka nchini India bali pia vimeongeza hasira na ghadhabu ya umma.

Mwaka 2012, mwanafuzi wa masomo ya udaktari mwenye umri wa miaka 23 alibakwa na kundi la wanaume sita ndani ya basi katika mji wa New Delhi. Baadaye alifariki dunia kutokana na majeraha ya ndani akiwa hospitali.

Tukio hilo liliamsha maandamano ya umma yaliyotikisa nchi nzima yakitaka kuwekwa kwa sheria kali dhidi ya wahalifu wa vitendo vya ubakaji.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment