WAASI: OBAMA AMETUANGUSHA



WAASI nchini Syria wanasema kuwa wanahisi kuwa wameangushwa na Rais Barack Obama kutokana na uamuzi wake wa kulizingatia pendekezo la Urusi linalokusudia kuutafuta suluhu ya kidiplomasia mgogoro wa nchi hiyo uliodumu kwa miaka miwili na nusu.

Jana Jumatano, wapiganaji kadhaa walielezea ghadhabu yao kutokana na uamuzi wa Washington kusimamisha kwa muda suala la vita na kuipa nafasi demokrasia.

"Watu walikuwa wana matumaini kuwa Marekani itafanya mashambulizi yatakayoleta suluhisho, lakini tulitarajia kuwa hakuna mbacho kingetokea kwa sababu hakuna mwenye suluhu kwa mgogogro wa Syria,” walisema wapiganaji hao.

Siku moja kabla, Muungano wa Baraza la Kitaifa la Syria (SNC) ulisema katika taarifa yake kuwa Marekani inapaswa kuendelea na mpango wake wa kuishambulia Syria ili kuwapa waasi hao nafasi ya kushinda vita dhidi ya serikali ya Rais Bashar al-Assad.

Shinikizo la kuishambulia Syria liliongezeka baada ya serikali ya Assad kuhuhumiwa kuwa ilitumia silaha za kemikali kwenye viunga vya mji wa Damascus tarehe 21 Agosti.

Hata hivyo, serikali ya Damascus imekanusha vikali madai hayo na kusema kuwa waasi ndio waliotumia silaha hizo za sumu ili kuamsha moto wa hasira dhidi ya utawala wa Bashar.

Juzi Jumanne, Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria, Walid al-Muallem, alisema kuwa serikali ya Damascus iko tayari kutekeleza pendekezo lililotolewa na Urusi la kuyaweka maghala ya silaha za kemikali chini ya udhibiti wa Umoja wa Mataifa.

Serikali ya Urusi ilitoa pendekezo hilo wakati wa mkutano baina ya Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi, Sergei Lavrov na waziri Muallem mjini Moscow Jumatatu iliyopita.

"Tunataka kuingia katika mkataba wa kupiga marufuku silaha za kemikali. Tuko tayari kutekeleza wajibu wetu kulingana na mkataba huo, ikiwemo kutoa taarifa zote kuhusu silaha hizi,” alisema Muallem.

Katika kujibu hatua hiyo, Rais wa Marekani aliliomba bunge la Congress la nchi yake kuakhirisha zoezi la upigaji kura ya kuidhinisha vita dhidi ya Syria ili kulipa nafasi pendekezo la Urusi.  


Syria imekuwa katika machafuko makubwa tangu Machi 2011 na zaidi ya watu 100,000 wameshapoteza maisha yao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment