VIFO VYAONGEZEKA ZAIDI HUKO NAIROBI

Kenya Defense Forces (KDF) arrive on September 22, 2013 at the Westgate mall in Nairobi.
Askari wa jeshi la Kenya (KDF) wakiwasili kwenye kituo cha biashara cha Westgate leo.


IDADI ya vifo kutokana na shambulizi lililofanywa na wanamgambo wa Kisomali kwenye kituo kimoja cha biashara mjini Nairobi imeongezeka na kufikia watu 59 huku idadi rasmi ya wale wanaoendelea kushikiliwa mateka ikiwa haijulikani.

Leo Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya, Joseph Ole Lenku alisema: “Bado kuna watu wanaoshikiliwa mateka ndani ya maduka haya, na hili linafanya kazi hii kuwa ngumu. Mpaka sasa kuna watu 59 waliouawa.”

Vile vile, Lenku alithibitisha kuwa kwa uchache watu 175 walijeruhiwa katika shambulizi hilo lililoanza jana majira ya saa 5 asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki.

Lenku aliongeza kuwa takriban watu 1,000 wameshaokolewa, lakini bado kuna idadi ya mateka ambao wanashikiliwa na watekaji ndani ya kituo hicho cha Westgate.

“Kuna washambuliaji kadhaa ambao bado wapo katika jengo, na idadi yao inakadiriwa kuwa kumi mpaka kumi na tano,” alisema waziri huyo.

“Tunaamini kuna watu ambao bado wapo ndani ya jengo hilo, ndiyo maana operesheni hii inakuwa ngumu.”

Polisi pamoja na vikosi vya jeshi la Kenya vinaendesha operesheni maalumu kumaliza mzingiro huo.

Msemaji mmoja wa kundi la al-Shabab alisema katika taarifa iliyotolewa jana usiku kuwa kundi lake ndilo lililohusika na shambulizi hilo.

Mapema jana Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, aliahidi “kuwasaka washambuliaji hao kokote watakapokimbilia.”

Mwaka 2011 Kenya ilituma askari 4,000 kusini mwa Somalia kwenda kuisaidia serikali ya nchi hiyo katika mapambano yake dhidi ya wapiganaji wa al-Shabaab.


Askari hao wa Kenya ni sehemu ya Kikosi cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) kinachopata mafunzo na zana kutoka nchi wahisani kwa lengo la kurejesha usalama nchini humo.v
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment