MUGABE: WABAKAJI WAHASIWE


RAIS Robert Mugabe amesema kuwa serikali inatakiwa kuweka adhabu kali zaidi kwa wabakaji na kupendekeza kuwa waleo wanaowabaka watoto wahasiwe, akieleza kuwa hatua kali inatakiwa kuchukuliwa kukabiliana na tatizo hilo linaloshamili.

Akizungumza baada ya ufunguzi rasimi wa Bunge siku ya Jumanne, Mugabe alielezea kusitishwa kwake na ongezeko la matukio ya watu wazima kuwanajisi watoto na kusema kuwa hatua hiyo itasaidia kukabiliana na matukio hayo.


“Tutawawekea adhabu kali sana, hatukubali kabisa watoto na wanawake kunajisiwa” alisema.

Mugabe alisema kuwa ni wakati wa kufikiria kuweka adhabu kali zaidi akiongeza kuwa alikuwa tayari kuweka adhabu ya kuwahasi wabakaji.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment