BRAZILI KUTUMIA KIKOSI CHA USALAMA WA TAIFA KUWADHIBITI WAANDAMANAJI

Riot police face off against demonstrators during protests against poor public services, police violence and government corruption, in Sao Paulo June 18, 2013 (Reuters / Alex Almeida)
Polisi wakikabiliana na waandamanaji katika maandamano ya kupinga huduma mbovu za kijamii, unyanyasaji wa polisi na ufisadi wa serikali mjini Sao Paulo Juni 18, 2013



Serikali ya Brazili itatumia Kikosi cha Usalama wa Taifa vyenye silaha nzito katika miji mitano inayotarajiwa kutumika kwa mashindano ya kimataifa ya Soka katika juhudi za kudhibiti maandamano yanayoendelea katika nchi hiyo.

Tangazo hilo lililotolewa na Wizara ya Sheria linakuja baada ya siku moja ya makabiliano makali baina ya waandamanaji na na jeshi la polisi.

Kwa kawaida kikosi cha usalama wa taifa nchini Brazili hutumika kushughulikia migogoro nyeti ya kiusalama, kama vile maasi ya wafungwa au vurugu kubwa za magenge ya kihalifu.

Maandamano hayo yalizuka mapema mwezi huu kutokana na kupanda kwa gharama za usafiri wa umma na kuibua vuguvugu kubwa dhidi ya serikali, huku maelfu ya watu wakiandamana kuonesha hasira yao dhidi ya sera za serikali.


Demonstrators run past burning garbage during protests against poor public services, police violence and government corruption in Sao Paulo June 18, 2013 (Reuters / Alex Almeida)
Waandamanaji wakipita karibu na takataka zinazoungua katika maandamano ya kupinga huduma mbovu za kijamii, unyanyasaji wa polisi na ufisadi wa serikali mjini Sao Paulo Juni 18, 2013

Gharama kubwa za kuandaa mashindano ya Kombe la Dunia nchini humo ni miongoni mwa masuala yaliyoibua maandamano hayo – waandamanaji wanasema kuwa bora pesa hizo zingetumika kutatua matatizo yanayoikabili jamii, badala ya kuzitumia kwenye tukio moja la kimichezo.

Jana Jumanne Rais wa Brazili, Dilma Rousseff alijaribu kutuliza joto la maandamano, akasema kuwa serikali yake inawajali raia na inataka kuyafanyia kazi manung’uniko ya waandamanaji. “Kiwango cha maandamano ya jana kinaonesha nguvu ya demokrasia yetu, nguvu ya sauti za waandamanaji na uzalendo wa wananchi wetu,” alisema katika hotuba iliyooneshwa katika vituo vya televisheni.

Aliendelea kulaani matukio ya ghasia na kuwataka waandamanaji waandamane kwa amani.

Riot polce take positions during a protest in Sao Paulo, Brazil on June 18, 2013 (AFP Photo / Daniel Guimaraens)
Polisi wakijipanga wakati wa maandamano mjini Sao Paulo, Brazili, Juni 18, 2013

Students try to break down a door of the City Hall building in Sao Paulo, Brazil on June 18, 2013 (AFP Photo / Miguel Schincariol)
Wanafunzi wakijaribu kuvunja mlango wa jengo la Ukumbi wa Jiji mjini  Sao Paulo, Brazili Juni 18, 2013 



People gather at the September 7 square on June 18, 2013 in Belo Horizonte, state of Minas Gerais (AFP Photo / Douglas Magno)
Wananchi wakiwa wamekusanyika kwenye medani maarufu ya September 7  mnamo Juni 18, 2013 mjini Belo Horizonte, katika jimbo la Minas Gerais 
Students take part in a demonstration at Praca da Se, in Sao Paulo, Brazil on June 18, 2013 (AFP Photo / Miguel Schincariol)
Wanafunzi wakishiriki maandamano katika eneo la Praca da Se, mjini Sao Paulo, Brazil Juni 18, 2013

Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment