AMUUA MUMEWE KWA SABABU YA MAHARI


Mwanamke mmoja amempiga na kumuua mumewe katika eneo la Barsaloi, Samburu, nchini Kenya baada ya kutofautiana kuhusu mahari ya mabinti zao wawili.
Mwanamke huyo alimuua mumewe, ambaye ni chifu msaidizi, Jumanne usiku.
Mkuu wa polisi ya Samburu kati, OCPD Morris Assila alisema kuwa naibu huyo wa chifu alikuwa amepewa mahari ya mabinti zao wawili lakini hakumpa mkewe fungu lake kulingana na mila na desturi za Wasamburu.
Mgogoro uliibuka na wanandoa hao wakapigana na hapo ndipo mke alipomuua mume. 
Assila anasema kuwa mwanamke huyo ametiwa nguvuni na atafikishwa mahakamani. 
Mwili wamarehemu umepelekwa katika hospitali ya Wilaya ya Maralal kwa ajiliya kuhifadhiwa.
CHANZO: STANDARD DIGITAL

Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment