Mtoto wa Kipalestina aliyejeruhiwa akiwa amelala katika kitanda cha hospitali kufuatia shambulizi la anga la majeshi ya Israeli katika eneo la Beit Lahia, kaskazini mwa Ukanda wa Gaza leo Novemba 17, 2012. Mashambulizi ya ndege za Israeli yalipiga makao makuu ya baraza la mawaziri wa serikali ya Hamas mjini Gaza, huku mashuhuda wakiripoti kutokea kwa hasara kubwa katika jengo hilo. AFP
Binti wa Kipalestina akilia wakati wa mazishi ya Audi Naser, aliyeuawa na mashambulizi ya ndege za Israeili. Alizikwa katika eneo la Beit Hanun, kasikazini mwa Ukanda wa Gaza Strip, Novemba 16, 2012.
Ndani ya siku nne, katika Ukanda wa Gaza, Wapalestina 41 wameuawa, wakiwemo watoto 11, na mwanamke mjamzito aliyetegemea kujifungua mapacha. Zaidi ya watu 400 wamejeruhiwa, wengi wao vibaya sana.







0 comments:
Post a Comment