PALESTINA YAFUNGUA UBALOZI VATICAN

Palestine opens embassy to the Vatican  


VATICAN CITY

Katika hatua inayoonekana kuwa ya kihistoria, Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amefungua ubalozi wa nchi yake mjini Vatican.

"Leo tulikutana na Papa Francis. Ni matumaini yangu kuwa mataifa mengine yatafuata mfano wa Vatican na kulitambua taifa na dola ya Palestina," Abbas aliwaambia waandishi wa habari baada ya sherehe ya ufunguzi wa umbalozi huo unaopatikana katika Mtaa wa Porta Angelica.

Vatican iliitambua Palestina kama taifa na dola mwaka 2005.

Kuhusu ahadi yenye utata ya Rais mteule wa Marekani Donald Trump kuwa atauhamisha ubalozi wa Marekani kutoka mjini Tel Aviv kwenda eneo linalokaliwa kimabavu la Jerusalem Mashariki, Abbas alisema kuwa hatua hiyo itakuwa na madhara kwa mchakati wa amani.

"Tunasubiri kuona kama itatokea. Ikitokea, haitasaidia suala la amani na ni matumaini yetu kuwa haitatokea," alisema.

Baada ya kauli yake hiyo, Abbas aliingia katika ubalozi huo mpya na kupandisha bendera ya Palestina.

Askofu mkuu Angelo Becciu alihudhuria shughuli hiyo akiiwakilisha Vatican.

Jumapili ya leo Ufaransa inatarajiwa kuandaaa mkutano wa kimataifa mjini Paris unaolenga kufufua majadiliano kati ya pande mbili za mgogoro wa Mashariki ya Kati.

Wakati utawala wa Israel ukidai kuwa Jerusalem Mashariki ni “mji mkuu wake wa milele” baada ya kuukalia kwa mabavu wakati wa vita vya mwaka 1967, jumuiya ya kimataifa haitambui madai hayo, na balozi za kigeni ziko mjini Tel Aviv.

Baada ya uhusiano mbaya kati ya Rais wa Marekani anayeondoka Barack Obama na Waziri Mkuu wa utawala wa Israel Benjamin Netanyahu, kuna wasiwasi wa namna utawala wa Trump utakavyoathiri uhusiano kati ya Marekani na Israel ambao ni washirika wa muda mrefu.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment