NDEGE YALAZIMIKA KURUDI ILIKOTOKA BAADA YA UGOMVI WA MKE NA MUME

 

Ndege moja ya Shirika la Ndege la Uturuki (Turkish Airlines) iliyokuwa ikitokea Istanbul kwenda Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro ililazimika kukatisha safari na kurudi Istanbul baada ya kuzuka mapigano kati ya mke na mume kwenye ndege.

Ndege hiyo iliyoondoka Istanbul saa 1: 30 kwa majira ya nchini Uturuki, ilipofika kwenye anga ya Cairo, abiria wawili raia wa Slovenia Anton Cestnik na mkewe Knavdiya Cesnit walianza kubishana na kuzozana. Cestnik aliwashambulia abiri wengine huku akiharibu skrini iliyokuwa upande wa nyuma wa siti.

Abiria wengine waliwataarifu wafanyakazi wa ndege kuhusu tukio hilol ambapo waliingilia kati lakini hawakuweza kumtuliza bwana huyo mwenye umri wa miaka 54. Rubani aliamua kurudi Istanbul huku wafanyakazi wa ndege wakiendelea kushughulika na abiria huyo wakamfunga pingu na kumpeleka eneo la nyuma ya ndege. Cestnik alikata pingu hizo za plastiki na kuendelea kuwashambulia abiria wengine.

Baada ya kutua katika uwanja wa Atatürk mjini Istanbul, Cestnik na mkewe walikabidhiwa mikononi mwa polisi ambapo abiria wengine 149 walianza safari kuelekea Dar es Salaam baada ya kuchelewa kwa muda wa saa 7. Katika maelezo yake mbele ya polisi, Cestnik alisema kuwa ana tatizo la hofu.

Katika taarifa yake, Shirika la Ndege la Utruki lilithibitisha kutoka kwa tukio hilo lakini halikufafanua zaidi. Kwa mujibu wa sheria za usafiri wa anga, wanandoa hao walirejeshwa kwenye kituo chao cha awali mjini Munich nchini Ujerumani, huku shirika hilo likimtoza faini Cestnik kwa hasara ambayo shirika hilo liliipata kutokana na tukio hilo.

CHANZO: Sabah Daily


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment