BALOZI ANDREY KARLOV NI NANI?

Balozi wa Russia nchini Uturuki aliyeuawa leo mjini Ankara.



Balozi wa Urusi nchini Uturuki bwana Andrey Karlov, ameuawa leo Jumatatu kwa kupigwa risasi na mtu mwenye silaha wakati akishiriki ufunguzi wa maonesho ya picha katika mji mkuu wa Uturuki, Ankara.

Karlov alizaliwa Februari 4 mwaka 1954 mjini Moscow, na akahitimu masomo yake mwaka 1976 katika Chuo cha Uhusiano wa Kimataifa cha mjini humo, ambapo mwaka 1992 alihitimu masomo yake katika Chuo cha Diplomasia kilicho chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi.

Karlov alianza maisha yake ya kidiplomasia mwaka 1976, ambapo alishika nafasi mbalimbali katika Wizara ya Mambo ya Nje ya iliyokuwa Muungano wa Kisovieti na Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Urusi, sambamba na majukumu mbalimbali ya nje ya nchi aliyokabidhiwa.

Alifanya kazi katika ubalozi wa Muungano wa Usovieti katika nchi ya Korea Kaskazini mwaka 1979, 1984, 1986 na 1991.

Alikabidhiwa jukumu la kuwa balozi wa nchi yake nchini Uturuki tangu mwaka 2013. Ameacha mjane na mtoto mmoja wa pekee.

Siku ya leo amepigwa risasi wakati akihudhuria maonesho ya sanaa za Kirusi mjini Ankara, tukio lililokatisha maisha yake.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment