AJALI YA NDEGE YA MIZIGO YAUA WATU WASIOPUNGUA 32

 


Ndege moja ya mizigo ya Kituruki iliyokuwa ikijaribu kutua katika uwanja mkuu wa ndege nchini Kyrgyzstan imeanguka katika kijiji kimoja na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 32.

Kwa mujibu wa uongozi wa uwanja huo, ndege hiyo iliyokuwa ikitoka Hong Kong kwenda Istanbul ilitakiwa kutua katika Uwanja wa Manas, nje kidogo ya mji mkuu Bishkek.

Wafanyakazi wa kikosi cha uokozi wameopoa mwili wa rubani na wanakijiji 15, wizara ya afya nchini humo imesema.

Chanzo hasa cha ajali hiyo ya ndege hiyo aina ya Boeing 747 inayomilikiwa na shirika la ndege la ACT, hakijajulikana.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment