MOHAMED ABOUTRIKA AWEKWA KWENYE ORODHA YA UGAIDI

Mohamed Aboutrika 


Kiungo mkongwe wa Misri, Mohamed Aboutrika, amewekwa kwenye orodha ya ugaidi nchini humo kwa kudaiwa kuunga mkono vuguvugu la Udugu wa Kiislamu lililopigwa marufuku.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38, ambaye aliwahi kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji wa mwaka inayotolewa na BBC kwa mwaka 2008 na ambaye aliichezea timu yake ya taifa michezo zaidi ya 100, anatuhumiwa kuwa miongoni mwa wafadhili wa chama hicho, ambacho serikali ya Misri inakiona kuwa ni cha kigaidi.

Aboutrika aliunga mkono waziwazi urais wa Muhammed Morsi wa chama hicho mwaka 2012. Morsi aliondolewa madarakani na jeshi la nchi hiyo mwaka mmoja tu baada ya kukalia kiti cha urais.

Mwaka 2015 mali kadhaa za Aboutrika zilishikiliwa na serikali, na sasa anakabiliwa na hatari ya kunyang’anywa pasipoti yake na kuzuiliwa kuondoka nchini humo.

Hata hivyo, mwanasheria wake, Mohamed Osman, ameashiria kuwa uamuzi huo utakatiwa rufaa na kwamba Aboutrika “hajatiwa hatiani au kupewa taarifa rasmi ya mashitaka yanayomkabili”.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment