AFCON: UGANDA KUMENYANA NA GHANA LEO

 UGANDA-CRANES-FANS


Timu ya taifa ya Uganda leo watashuka dimbani kuchuana na timu ya taifa ya Ghana katika uwanja wa Stade Sogara katika mji wa Port Gentil nchini Gabon ikiwa imepita miaka 39 tangu Uganda iliposhiriki katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Uganda wamewahi kukutana na Ghana katika mechi tatu ndani ya miaka mitatu iliyopita. Waghana hawakushinda mechi yoyote dhidi ya Uganda. Hata hivyo, mtifuano wa leo unatarajiwa kuwa na changamoto kwa Timu hiyo ya Uganda kutokana na ukweli kwamba Waghana wana uzoefu mkubwa na michuano hiyo.

“Tangu mwaka 1978, hatujashiriki AFCON mara 19 wakati Ghana imekuwa ikishiriki michuano hii kila mara. Hivyo, wanakuja uwanjani wakiwa na uzoefu mkubwa na michuano hii.” Kocha wa Uganda Micho Sredojevic aliambia Daily Monitor jana mchana kwenye makazi ya timu yake kwenye Hotel Du Parc, ambayo iko umbali wa dakika tatu kutoka dimba la Stade Sogara

Mlinzi wa timu ya Uganda, Murushid Juuko na Kiungo Khalid Aucho hawatocheza mecho hiyo ya kwanza kwa sababu wamesimamishwa.

Mkongwe wa soka la Zambia, Kalusha Bwalya, amewaambia Uganda Cranes wafanye juu chini wasipoteze mechi hii ya kwanza, akisema kuwa timu hiyo itakabiliana na timu kubwa na kusisitiza kwa kusema ‘ngoja tone namna Uganda watakavyoanza. Lakini ninawaambieni ni mechi ngumu. Misri, Ghana, Mali, sio timu za mchezo.’

“Mechi ya kwanza katika mashindano yoyote huwa ni mechi muhimu sana. Tunatakiwa kuingia dimbani kwa nguvu zote kwa sababu timu tunayopambana nayo ni Ghana. Hatuwazi kuhusu Misri na Mali; mipango na fikra zetu tunazielekeza kwa Ghana.” Alisema Kocha Micho.


“Tunajua kuwa taifa lote liko nyuma yetu na hii ni fursa ya kihistoria kwa baadhi yetu ambao tumekuwa katika kikosi hiki kwa muda mrefu. Hatutaki kuondoka tukiwa na majuto, hivyo kitu pekee cha kufanya ni kutumia uwezo wetu wote kutimizi matarajio ya Waganda wenzetu.” Alisema kiungo wa Cranes, Tonny Mawejje
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment