SENEGAL KUONGOZA KIKOSA CHA JESHI KUMUONDOA JAMMEH KWA NGUVU

Gambian President Yahya Jammeh listening to one of his aides in Banjul, during the closing rally of the electoral campaign. (AFP Photo)
Rais wa Gambia, Yahya Jammeh akimsikiliza mmoja wa wasaidizi wake mjini Banjul, wakati wa kufunga mkutano wa kampeni



Kiongozi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi amesema kuwa viongozi wa nchi hizo watatuma askari kwenda Gambia iwapo rais wa nchi hiyo aliyeshindwa uchaguzi hatoachia madaraka mwezi ujao.

Marcel de Souza amewaambia waandishi wa habari kuwa Jumuiya hiyo imeichagua Senegal kuongoza kikosi cha kijeshi iwapo Yahya Jammeh hatokabidhi madaraka Januari 19 ambayo ndio mwisho wa muhula wake kikatiba.

Akizungumza na wanahabari mjini Bamako nchini Mali, De Souza amesema kuwa bado Jumuiya hiyo inaendelea kutumia njia za kidiplomasia kumshawishi Jammeh akubali kuachia ngazi.

Jammeh aliingia madarakani miaka 22 iliyopita na amekuwa akituhumiwa kuwafunga na kuwatesa wapinzani wake.

Aliwashangaza Wagambia na dunia kwa ujumla alipokubali kushindwa uchaguzi lakini baadaye akabadili kauli.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment