MAKUBALIANO YAFIKIWA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO

The photo shows the Democratic Republic of the Congo’s President Joseph Kabila. Under a deal announced by the opposition, Kabila will remain in power for another year. (By AFP)
Rais Joseph Kabila



Serikali na upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamefikia muafaka wa makubaliano ambayo yatamrhusu Rais Joseph Kabila kubaki madarakani kwa mwaka mmoja zaidi kwa sharti la kutogombea muhula wa tatu, upinzani umesema.

“Kabila atabaki kwa mwaka mmoja zaidi,” kiongozi wa upinzani Martin Fayulu amesema leo Ijumaa na kuongeza kuwa “hatoruhusiwa kugombea muhula wa tatu.”

Mkataba huo kati ya pande mbili umekuja baada ya makumi ya watu kuuawa katika maandamano dhidi ya serikali yaliyofanyika wiki hii.  Umoja wa Mataifa umesema leo Ijumaa kuwa kiasi cha watu 40 waliuawa.

Msemaji wa serikali alikataa kutoa maelezo kuhusu kilichomo kwenye makubaliano hayo, ambayo yatahitaji kukubaliwa na wajumbe wote wa mazungumzo yanayosimamiwa na viongozi wa Kanisa Katoliki nchini humo.

Jean Marc Kabund ambaye ni katibu mkuu wa chama kikuu cha upinzani cha UDPS, alionya kuwa mkataba huo bado haujahitimishwa.

“Leo ni siku ya mwisho ya mazungumzo ,” alisema na kuongeza, “yanayoweza kufaulu au kuvunjika.”

Muhula wa pili wa Rais Kabila ulimalizika siku ya Jumanne. Kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo, rais mpya anatakiwa kuchaguliwa sasa. Hata hivyo, bwana Kabila ameendelea kubaki madarakani baada ya uchaguzi uliotakiwa kufanyika mwezi uliopita kuahirishwa kwa sababu ya kile ambacho serikali ilisema ni kutokamilika kwa zoezi la uandikishaji wa wapiga kura.

Picha iliyochukuliwa Desemba 20, 2016, ikiwaonesha watu wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya maandamano katika mtaa wa  Yolo mjini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.


Rais Kabila amekuwa akituhumiwa kufanya njama za kubaki madarakani. Hata hivyo, wafuasi wake wanasema kuwa anatekeleza matakwa ya kikatiba lakini kuondoka madarakani kunaweza kusababisha vita vya kugombea madaraka na kuyaweka maisha yake hatarini.

Baba yake, mzee Laurent Kabila, ambaye alikuwa rais wa nchi hiyo aliuawa mwaka 2001 na tangu wakati huo hakujawa na ubadilishanaji wa madaraka kwa njia ya amani.

Alichukua madaraka siku kumi baada ya kuuawa kwa baba yake.

Maandamano na mauaji ya wiki hii yameibua wasiwasi kwamba taifa hilo linaelekea kwenye ghasia na vurugu kubwa.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment