AFISA WA POLISI AKIRI KUMUUA BALOZI WA UGIRIKI NCHINI BRAZIL

The undated photo shows Greek Ambassador to Brazil Kyriakos Amiridis (C). (Photo by AFP)
Balozi wa Ugiriki nchini Brazil Kyriakos Amiridis (katikati)

Afisa mmoja wa polisi katika mji wa Rio de Janeiro nchini Brazil amekiri kumuua balozi wa Ugiriki nchini humo, yumkini kwa maelekezo ya mke wa balozi huyo ambaye yasemekana alikuwa na uhusiano naye wa kimapenzi, duru za polisi zimesema.


Kituo cha televisheni cha Global cha nchini humo kimenukuu duru hizo zikisema kuwa mapema Ijumaa mchana, afisa huyo aitwaye Sergio Moreira mwenye umri wa miaka 29, alikiri kumuua balozi Kyriakos Amiridis siku ya tarehe 26 Desemba.
Mke wa balozi huyo, aitwaye Francoise, ambaye ni raia wa Brazil, anashikiliwa na jeshi la polisi.


Wapelelezi wa jeshi la polisi wanasema kuwa waliamini kuwa Francoise na Moreira walikuwa wamepanga mauaji hayo, kituo hicho cha TV kilisema.
Jioni ya Alhamisi polisi waliukuta mwili ulioungua ndani ya gari iliyokuwa imekodishwa na Amiridis.


Polisi mjini humo wamekataa kutoa kauli yoyote kuhusu uchunguzi wao. Ubalozi wa Ugeriki mjini Brasilia, nao ulikataa kutoa kauli.


Mjini Athens, msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni wa Ugeriki, Stratos Efthymiou, alisema kuwa serikali haina kauli yoyote kwa sasa.


Mapema Alhamisi, polisi walithibitisha kuwa balozi huyo alikuwa ametoweka tangu Jumatatu usiku ambapo mara ya mwisho alionekana akiondoka nyumbani kwa familia ya mkewe katika kitongoji kimoja chenye ghasia nyingi mjini Rio.

Taarifa za kupotea kwake ziliripotiwa na mkewe siku ya Jumatano.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment