MLIPUKO WA BOMU WAUA ASKARI 13 UTURUKI

 


Kwa uchache askari 13 wameuawa na wengine 48 kujeruhiwa baada ya bomu lililotengwa kwenye gari kulipuka jirani na chuo kikuu cha Erciyes katika Mkoa wa Kayseri katikati mwa Uturuki, taarifa ya jeshi la nchi hiyo imesema ikiwa ni wiki moja baada ya shambulizi la mjini Istanbul lililoua watu 44.

Mlipuko huo ulitokea majira ya saa 2:45 asubuhi kwa majira ya eneo hilo wakati basi lililokuwa limebeba raia na askari waliokuwa wakitoka kazini lilipolipuliwa na bomu lililotengwa kwenye gari, jeshi limesema.

Jumamosi iliyopita, milipuko pacha ya mabomu nje ya uwanja wa soka katika mji wa Istanbul iliua kiasi cha watu 44 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 100.

Kundi la wanamgambo wa Kikurdi lijulikanalo kama Tai waanaopigania uhuru wa Kurdistan au TAK, lilidai kuhusika na mashambulizi ya Istanbul. Inaaminika kuwa TAK ni tawi la kundi la wapiganaji wa Kikurdi, maarufu kama PKK.

Serikali ya Uturuki imekuwa ikipambana vikali na kundi la PKK na makundi mengine ya Kikurdi, ambayo Ankara inayaona kama kitisho cha usalama na imeyaweka katika orodha ya makundi ya kigaidi.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment