MAHUSIANO: MAMBO MEPESI YANAYOMFURAHISHA MKE





1. Muachie ujumbe wa kimahabba nyumbani katika eneo asilolitarajia                       

2. Anapojipulizia manukato mwambie kuwa harufu yake ni nzuri                        

3. Mshukuru kwa huduma za nyumbani hata kama ni kidogo.                       

4. Msifu kwa mapishi yake na umwambie unavyoyahusudu. Usifanye hivyo mkiwa mezani, fanya baada ya kumaliza kula.

5. Iwapo kuna kifaa kimeharibika nyumbani kitengeneze                       

6. Usifu uzuri wa nywele zake                       

 7. Mkumbatie unapomkuta amehuzunika.                       

8. Msaidie kuondokana na wasiwasi.                       

9. Amiliana naye kwa huruma na upole anapokuwa katika siku zake

10. Shiriki katika kumfanya aonekane mzuri, hata kwa kumpendekezea nguo ya kuvaa.                       

11. Anzisha mazungumzo kuhusu upendo na mahabba                       

12. Mpe zawadi yenye kumkumbusha kuhusu wewe.                       

13. Mbusu kila unapoenda kazini                       

14. Mpatie msaada pindi anapouhitaji                       

15. Mshirikishe katika kufanya maamuzi.                       

16. Usimpe sababu za kumpa huzuni.                       

17. Mpe remote atazame filamu anayoipenda.                       

18. Mtegee sikio anapozungumza.

19. Usiwasifu wanawake wengine mbele yake.                       

20. Shirikiana naye katika michezo anayoipenda                       
21. Usiache kuwa karibu naye kimwili                        

22. Muite kwa majina matamu                       

23. Muombe radhi unapomkosea                       

24. Mchekeshe                       

25. Siku ya ndoa yenu ifanye kuwa siku muhimu sana                       

26. Mweleze wazi matatizo yanayokukabili                       


27. Usimlazimishe kufanya mapenzi kama hana utayari na hamu ya kufanya.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment