MLIPUKO KWENYE SOKO LA FATAKI WAUA WATU 29



Kwa uchache watu 29 wamepoteza maisha na wengine 70 kujeruhiwa katika mlipuko uliotokea kwenye soko la fataki nchini Mexico.

Mlipuko huo umetokea kwenye soko la fataki la San Pablito katika mji wa Tultepec, kilometa 32 kaskazini mwa mji mkuu Mexico City.

Idadi ya vifo inaweza kuongezeka kwa kuwa vikosi vya uokozi vinaendelea kuwatafuta waathirika katika eneo la mlipuko.

Askari wa zimamoto wakitembea katiktai ya vifusi vilivyoachwa na mlipuko uliotokea kwenye soko la fataki nchini Mexico  Desemba  20, 2016. 

Wanajeshi wamepelekwa eneo hilo ili kusaidia kuwahamisha na kuwapeleka majeruhi hospitalini kwa magari ya wagonjwa na helikopta.

Gavana wa jimbo la Mexico, Eruviel Avila, amesema kipaumbele kwa sasa ni kuwahudumia majeruhi.

Askari wa zimamoto akitembea katikati ya kifusi kilichosababishwa na mlipuko mkubwa kwenye soko la fataki nchini  Mexico , Desemba 20, 2016.

"Sauti ya milipuko ilianza kurindima nasi tulidhani kuwa ni kwenye warsha ya eneo jirani," mwananchi mmoja wa eneo hilo alinukuliwa na shirika la habari la AFP. "Majirani walisema kuwa walihisi kila kitu kinatikisika, lakini mimi sikubaini hilo kwa sababu nilikuwa nakimbia," alisema.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment