NDEGE YA LIBYA ILIYOTEKWA YATUA MALTA

Image result for 'Hijacked' Libyan plane lands in Malta 


Ndege iliyotekwa ya Shirika la ndege la Libya, Afriqiyah, aina ya Airbus A320 ambayo ilikuwa ikifanya safari za ndani imetua katika Uwanja wa Ndege wa Malta.

Mapema leo Waziri Mkuu wa Malta, Joseph Muscat, aliandika ujumbe katika akaunti yake rasmi ya Twitter kuwa ametaarifiwa kuwa ndege hiyo imetekwa.

"Nimetaarifiwa juu ya utekaji nyara wa ndege ya Libya inayofanya safari za ndani ambayo ilielekezwa Malta. Maafisa wa usalama na shughuli za dharura wako katika hali ya utayari," aliandika Waziri Mkuu huyo.

"Ndege ya Afriqiyah kutoka Sabha kwenda Tripoli ilielekezwa na kutua Malta. Maafisa wa huduma za usalama wanafanya mawasiliano na watekaji," ulisomeka ujumbe huo.

Dauru kutoka ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa nchini Libya zinasema kuwa mazungumzo yanaendelea ili kuhakikisha kuwa abiria wote wanakuwa salama.

Watekaji wawili waliwatisha marubani kuwa wamebeba mabomu, wakawalazimisha kutoka nchini Malta badala ya uwanja wa Mitiga mjini Tripoli.

Utambulisho wa watekaji hao haujawekwa wazi. Inasemakana wamekubali kuweka chini silaha zao.



Duru za serikali ya Malta zinasema kuwa ndege hiyo ilikuwa imebeba watu 118, wakiwemo wafanyakazi saba wa ndege. Taarifa zinasema kuwa abiria wameachiwa huru.


Tangu mwaka 2011, Libya imekuwa katikati ya ghasia kufuatia mapinduzi yaliyomuondoa madarakani kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, Muammar Gaddafi, ambaye baadaye aliuawa. Aidha, Umoja wa Kujihami wa nchi za Magharibi, NATO, ulijiingiza katika mgogoro huo.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment