BURUNDI YAHAMA KUTOKA ANALOGIA KWENDA DIGITALI

 burundi-2

“Kuanzia leo na kuendelea, tukiwa na nia ya kutekeleza wajibu wetu wa kimataifa wa Mkataba wa Geneva wa mwaka 2006 ambao Burundi iliusaini, nchi yetu itahama hatua kwa hatua kutoka kwenye matangazo ya analogia kwenda kwenye digitali”, amesema Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza katika hotuba yake aliyoitoa katika sherhr ya uzinduzi wa matangazo ya televisheni kwa mfumo wa digitali kwenye ofisi za Televisheni ya Taifa la Burundi leo asubuhi ya tarehe 19 Desemba 2016, kama ilivyoripotiwa na mtandao wa IWACU.

Rais huyo aliomba radhi kwa serikali yake kushindwa kuhamia mfumo wa matangazo ya digitali tarehe 17 Juni 2015, ambayo ndiyo iliyokuwa tarehe ya mwisho.

Waziri wa mawasiliano, habari na teknohama wa nchi hiyo, Nestor Bankumukunzi, alisema kuwa maendeleo hayo yamefikiwa kutokana na mkopo kutoka Benki ya Exim ya China na ahadi ya ving’amuzi iliyotolewa na China.



Mabadiliko hayo yatakuwa ya hatua kwa hatua yakianza na Mkoa wa Bujumbura, eneo la katikati mwa nchi na hatimaye kuenea nchi nzima.


Aidha, Rais wa Burundi alizindua utandazaji wa miundombinu ya Mkongo (Fiber Optics) kwa eneo la Bujumbura, hatua itakayosaidia kupatikana kwa mawasiliano ya kasi katika taasisi za serikali kama vile Ikulu, Bunge, Seneti, hospitali na mahakama.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment