UCHAGUZI WA BUNGE LIBYA BILA GADDAFI




Raia wa Libya leo wamemiminika kwenye vituo vya kupigia kura kuwachagua wagunge katika uchaguzi unaotazamwa kama muhimu sana kwa mustakbali wa taifa hilo ambalo limekumbwa na mizozo ya kisiasa na ghasia za vita na mapigano.

Uchaguzi wa leo wa kuwania viti 200 vya bunge ni wa pili tangu kuanguka kwa utawala wa aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi mwaka 20011.

Aidha, uchaguzi huo unatazama kama hatua muhimu katika safari ya Libya kuelekea kwenye utawala wa kidemokrasia na uthabiti wa kisiasa.

Wagombea wapatao 2,000 wanachuana kuingia katika bunge jipya ambalo litaitwa Bunge la Wawakilishi.

Uchaguzi huo unafanyika bila chama chochote cha kisiasa. Katika juhudi za kuondosha minyukano ya kisiasa ndani ya vyama, ambayo ilidhoofisha uchukuliwaji wa hatua za maamuzi muhimu na kusababisha mzozo baina ya mawaziri wakuu wawili mahasimu mwezi Mei, wagombea wanawania nafasi hizo kama wagombe huru badala ya kuwakilisha vyama.

Nchi hiyo inahitaji serikali na bunge linalofanya kazi ili kuwa na nguvu dhidi ya wanamgambo wenye silaha, ambao walisaidia kumuondoa Kanali Gaddafi lakini kwa sasa wanakataa kuweka silaha chini na hawaitambui mamlaka yoyote.

Aidha, Libya inakabiliwa na mgogoro wa kibajeti kutokana na wimbi la maandamano kwenye viwanda vya mafuta na hatua ya wanamgambo kuyasshikilia maeneo muhimu ya uzalishaji na hivyo kuzorotesha uzalishaji wa nishati hiyo ambayo ni uti wa mgongo wa nchi hiyo.

Wakati huo huo, wananchi wa Libya wanahofia kwamba uchaguzi huo unaweza kuzalisha bunge lingine la mpito. Tume maalumu iliyopewa jukumu la kuandaa rasimu ya katiba mpya haijakamilisha kazi yake na hivyo kuacha maswali mengi juu ya aina ya mfumo wa kisiasa utakaofuatwa na taifa hilo.


Uchaguzi huo umeitishwa mwezi mmoja baada ya serikali kudai kuwa jenerali mmoja wa jeshi wa zamani alikuwa akipanga kufanya mapinduzi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment