Rais Barack Obama amesema kuwa askari 275 wa Kimarekani
wamepelekwa nchini Iraq ili kuulinda ubalozi wa Marekani na raia wake nchini
humo.
Mapema Jumapili wizara ya mashauri ya kigeni ya nchi
hiyo ilitangaza kitumwa kwa kikosi hicho lakini haikutaja ukubwa wake.
Katika barua yake kwa uongozi wa bunge la Congress, Rais
Obama amesema kuwa kuanzia Juni 15 askari hao walianza kusambaa kwenye maeneo
mbalimbali ya Iraq kwa lengo la kuwalinda wafanyakazi wa Kimarekani na ubalozi
wake mjini Baghdad.
Aidha, Rais Obama ameashiria kuwa kikosi hicho
kitaendelea kubaki Iraq kadiri itakavyohitajika.
Leo Rais Obama anatarajiwa kufanya kikao na jopo lake la
masuala ya usalama kudurusu hali ya kuzorota kwa usalama nchini Iraq, kuangalia
hatua inayopaswa kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kufanya mashambulizi ya ndege
kuwazuia wanamgambo wanaoishikilia miji kadhaa mashariki mwa Iraq.
0 comments:
Post a Comment