MAUAJI MENGINE KENYA

 

Maiti nane zimepatikana katika eneo la Poromoko karibu na mji wa Mpeketoni nchini Kenya kufuatia mashambulizi mapya usiku wa kuamkia leo. Nyumba kadhaa zimechomwa katika mashambulizi hayo, kwa mujibu wa polisi na wakazi wa eneo hilo. Kuna taarifa kuwa kundi la Alshabaab, kupitia kituo chake cha radio Andalus, kimedai kufanya shambulizi hilo na kwamba wamewaua watu 20. Idadi ya vifo inaweza kuongezeka kwa kuwa polisi na wakazi wa eneo hilo wanaendelea kutafuta miili mingine. Wakazi wengine wanasema kuwa nyumba zimechomwa katika eneo la Mapenya usiku wa kuamkia leo.


Mkuu wa polisi nchini humo, David Kimaiyo, amethibitisha ripoti za kugunduliwa maiti hizo lakini akasema kuwa haijulikani iwapo mauaji hayo yametokana na mashambulizi mapya kama ilivyodaiwa na wakazi. Mpaka sasa hakuna watu waliokamatwa kufuatia mauaji ya zaidi ya watu 50 yaliyofanywa na watu wenye silaha usiku wa kuamkia jana katika eneo la Mpeketoni na Kibaoni.


Wakuu wa usalama wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Joseph Ole Lenku wako mjini Lamu na maafisa wengine wa usalama wamepelekwa katika eneo hilo.


CHANZO: KTN



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment