MAKAMU WA RAIS AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KASHFA YA UFISADI

 

Makamu wa Rais wa Argentina Amado Boudou ameitwa mahakamani na kesi yake kusikilizwa kwa muda wa saa tano kwa tuhuma za kuhusika ufisadi unaojumuisha kashfa ya na umiliki wa kampuni binafsi iliyoidhinishwa kuchapisha vitabu vya benki. Ripoti zinaashiria kuwa jaji ana ushahidi wa kutosha kumtia hatiani.

Kutokana na taathira ya kesi hii, maofisa wa serikali walielezea matumaini yao kwamba jaji ataruhusu mwenendo wa kesi hiyo kuoneshwa moja kwa moja na vituo vya televisheni.

Boudou alipowasili mahakamani, alilakiwa na maelfu ya wafuasi wake, ambao wanadai kuwa tuhuma hizo ni sehemu ya kampeni ya vyombo vya habari dhidi yake na kuivuruga serikali.

Baada ya kiongozi huyo kutoa ushahidi wake uliochukua masaa kadhaa, Jaji Jorge Lijo hakutoa hukumu bali alitaka waitwe watetezi wengine kutoa ushahidi zaidi kuhusu kadhia hiyo kabla ya kutoa uamuzi wa mwisho.

Wakati bwana Boudou akiondoka mahakamani alitoa ufafanuzi kuhusu mwenendo wa kesi hiyo. Uamuzi wa jaji umetoa nafuu kwa serikali ya rais Cristina Fernandez de Kirchner. Kwa sasa mahakama ina siku 10 kabla ya kutoa uamuzi dhidi ya kesi hiyo na mustakbali wa Makamu huyo wa Rais umegubikwa na giza nene.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment