MAANDAMANO KUPINGA VITENDO VYA WANAJESHI WA UFARANSA KUWABAKA WAKIMBIZI

 

Maandamano yamefanyika katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris, kutaka sheria ichukue mkondo wake dhidi ya askari wa Ufaransa wanaotuhumiwa kufanya vitendo vya ubakaji dhidi ya wakimbizi wakati wa mauaji ya kimbari ya Rwanda miongo miwili iliyopita.

Waandamanaji hao wamechukua hatua hiyo huku jeshi la Ufaransa likishtakiwa kwa ubakaji wa umati dhidi ya wakimbizi wa Rwanda, ambao askari wa Ufaransa walitakiwa kuwalinda wakati wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Mashitaka hayo yanaeleza kuwa askari katika kambi iiyokuwa ikilindwa na wanajeshi wa Ufaransa walikuwa wakiwachagua wanawake wa Kitutsi na kuwabaka zaidi ya mara moja.

Wanawake na askari hao hawajatangazwa hadharan, lakini waathirika wameshatambuliwa mahakamani. Kesi hiyo imekuwa ikiendelea kwa zaidi ya muongo mmoja sasa.

Mauaji ya kimbari ya Rwanda yalianza kufuatia kutunguliwa kwa ndege ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Juvenal Habyarimana Aprili 6, 1994. Rais wa Burundi Cyprien Ntaryamira naye aliuawa katika tukio hilo. Marais wote wawili walikuwa kutoka kabila la Wahutu.

Baada ya tukio hilo, Wahutu ambao walikuwa wengi, walianza kuwashambulia Watutsi. Mauaji hayo yalidumu kwa takriban siku 100 ambapo kiasi cha watu 800,000 waliuawa.




Mara kwa mara Ufaransa imekuwa ikikanusha kuhusika na mauaji hayo ya kimbari licha ya uchunguzi wa tume ya MUCYO ya Rwanda uliofanyika mwaka 2008 kubaini kuwa Ufaransa inadaiwa kutoa mafunzo kwa wapiganaji waliotekeleza mauaji hayo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment