BANGLADESH YAWAHUKUMU ADHABU YA KIFO WANACHAMA WA CHAMA CHA KIISLAMU



Mahakama nchini Bangladesh imewahukumu adhabu ya kifo wanachama wanane wa chama cha Kiislamu baada ya kudaiwa kuhusika na shambulizi la bomu la mwaka 2001 lililoua watu kumi.

Wakati akitoa hukumu hiyo leo, Jaji Ruhul Amin alisema kuwa shambulizi hilo lilifanywa kwa lengo la kuivuruga nchi na kuzusha tafrani.

Alisema kuwa mkuu wa kundi lililopigwa marufuku la Harkat-ul-Jihad al Islami (HUJI), Mufti Abdul Hannan, naye ni miongoni mwa washitakiwa.

Wanachama hao walishtakiwa kwa tuhuma za kutekeleza shambulizi la bomu katika maadhimisho ya mwaka mpya wa Kibengali mwaka 2001 katika mji mkuu wa nchi hiyo, Dhaka.

Aidha, mahakama hiyo imewahukumu adhabu ya kifo watu wengine sita kwa tuhuma za kutekeleza mashambulizi mawili ya mabomu yaliyojeruhi watu kadhaa.


Hata hivyo, wakili wa upande wa utetezi, bwana Faruque Ahmed amesema kuwa washtakiwa walikiri kufanya makosa baada ya kushurutishwa na kuadhibiwa na polisi wakati wa kuwahoji na ameahidi kukata rufaa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment