KENYATTA: AL-SHABAAB HAWAKUHUSIKA NA MAUAJI YA MPEKETONI

 

RAIS wa Kenya, Uhuru Kenyatta, ameyatupilia mbali madai kwamba shambulizi la Mpeketoni lililoua watu zaidi ya 50 liliendeshwa na kundi la Al shabab. Amesema kuwa shambulizi hilo ni la kikabila lililopangwa na kuandaliwa vizuri kwa kuwahusisha wanasiasa wa ndani ya nchi hiyo.

“Kuna wanasiasa wa ndani ambao wamekuwa wakieneza propaganda za kikabila na kampeni za chuki katika siku za hivi karibuni,” alisema.

Katika hotuba yake kwa taifa hilo iliyorushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni, Rais Uhuru aliahidi kuwashughulikia wanasiasa hao na wale wote waliozembea katika majukumu yao. “Maofisa wote wa usalama waliozembea majukumu yao wakati wa shambulizi hilo wamesimamishwa na watafikishwa mahakamani. Tabia hii haikubaliki kabisa,” alisisitiza Rais Kenyatta.

"Ninawatolea wito Wakenya wote wasisahau tunu zetu na wasisahau tulikotoka. Sitaruhusu kuona Kenya ikirudi tulikotoka,” aliongeza. “Serikali yangu itafanya kazi kwa ajili ya Wakenya wote popote watakapokuwa,” aliongeza katika kuhitimisha hotuba yake.

Alisema serikali yake itagharamia huduma zote za mazishi ya wale walioathiriwa na shambulizi hilo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment