JUAN MANUEL SANTOS ASHINDA KATIKA UCHAGUZI WA COLOMBIA

Colombia’s President Juan Manuel Santos celebrates after winning re-election in Bogota, June 15, 2014.
Rais wa Colombia Juan Manuel Santos akisherehekea baada ya kushinda uchaguzi mji  Bogota, Juni 15, 2014.



Matokeo rasmi yanaonesha kuwa Rais Juan Manuel Santos wa Colombia ametetea nafasi yake katika marudio ya uchaguzi yaliyofanyika hivi karibuni na hivyo kuendelea kuiongoza nchi hiyo kwa mhula wa pili.

Takwimu kutoka tume ya uchaguzi ya nchi hiyo zimeonesha kuwa bwana Santos ameshinda kwa asilimia 50.95 ya kura, huku mpinzani wake wa mrengo wa kihafidhina Oscar Ivan Zuluaga akifuatia kwa asilimia 45. Asilimia 4.03 ya kura ziliharibika.

Ushindi wa bwana Santos unatazamwa kama kibali cha kuendelea na mazungumzo ya amani na waasi wa (FARC). Santos aliwataka wananchi wa Colombia kuchagua kati ya “mwisho wa vita au vita visivyokuwa na mwisho.”

Mpinzani wake bwana Zuluaga, ambaye kwa muda mrefu amekuwa akipinga mazungumzo hayo ya amani, katika kampeni zake alitaka yawekwe masharti magumu kama sharti la kufikia kwa muafaka wowote.

Santos anasema kuwa anatarajia muafaka wa mzozo huo utasainiwa mwishoni mwa mwaka huu.

Serikali ya Colombia na waasi wa FARC wamekuwa wakifanya mazungumzo ya amani katika mji mkuu wa Cuba, Havana, tangu Novemba 2012, katika jitihada za kujaribu kukomesha mgogoro huo uliodumu kwa miongo mingi.

Kundi la FARC ndio kundi la muda mrefu zaidi katika eneo la Amerika ya kusini na limekuwa likipigana na serikali tangu mwaka 1964. Kundi hilo linaelezewa kuwa na wapiganaji wapatao 8,000 wanaofanya harakati zao katika misitu ya mashariki mwa taifa hilo.

Serikali ya Colombia inakadiria kuwa watu 600,000 wameuawa na wengine zaidi ya 4.5 wamelazimika kuyakimbia makazi yao kutokana na vita.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment