SPIKA WA BUNGE ATEKWA

 


Askari wa Israeli wamemteka Spika wa Bunge la Palestina Aziz Dweik katika wimbi jipya la kamatakamata inayoendelea kuhusiana na madai ya kutoweka kwa vijana watatu wa Kiyahudi.

Dweik, ambaye ni mwanachama wa chama cha Hamas amekamatwa na jeshi la Israeli leo katika Ukingo wa Magharibi.

Mpaka sasa zaidi ya Wapalestina 150 wamekamatwa kwa kisingizo hicho cha kutoweka kwa vijana hao. Israel inadai kuwa walitoweka siku ya Alhamisi katika eneo la Ukingo wa Magharibi na kulituhumu kundi la Hamas kuwa limewateka.

Hamas imekanusha madai ya Israel ikisema kuwa utawala wa Tel Aviv unakusudia kuhujumu mkataba wa maridhiano uliofikiwa kati ya kundi hilo na chama cha Fatah uliopelekea kuundwa kwa serikali ya Umoja wa Kitaifa ikiyahusisha makundi yote ya Kipalestina.

Msemaji wa Klabu ya Wafungwa wa Kipalestina, Amani Sarahna, amesema kuwa watu 60 walikamatwa jana, akaongeza kuwa kamatakamata bado inaendelea katika katika mji wa al-Khalil (Hebron) katika Ukingo wa Magharibi.

Mapema jana Jumapili, vikosi vya Israeli viliwakamata viongozi wa Hamas Hassan Yousef, Wasfi Qabaha, Khalid Abu Arafeh na Mohammed Totah.


Aidha, Israel imefunga kivuko cha mpaka cha Kerem Shalom ambacho hutumika kupeleka nishati ya mfuta katika eneo la Ukanda wa Gaza kufuatia kutoweka kwa walowezi hao. Kivuko cha Kerem Shalom ndio njia pekee ambayo hutumiwa na magari ya mafuta kuingiza nishati hiyo katika eneo hilo lililowekewa mzingiro.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment