‘MJANE MWEUPE’ ALIKUWA AMEOLEWA NA ASKARI WA KENYA

 A photo of Samantha Lewthwaite taken from her fake South African passport.

Samantha Lewthwaite, the ‘Mjane Mweupe’ anayesakwa kwa kushukiwa kuongoza shambulizi la Nairobi, ni mke au alikuwa ameolewa kwa siri na afisa wa zamani wa Jeshi la Wanamaji la Kenya, gazeti moja limenukuu taarifa za siri kutoka Polisi ya Uingereza, Scotland Yard.

Mumewe mpya ni Bwana Abdi Wahid, ambaye gazeti hilo limesema kuwa kwa sasa yupo Ulaya.

Hata hivyo, Inspekta Jenerali David Kimaiyo anasema kuwa hawakuwa wakijua kwamba “Mjane Mweupe” alikuwa ameolewa na askari wa zamani wa jeshi la Kenya.

“Hivi sasa ndiyo ninalisikia hili. Tunachojua ni kwamba alikuwa akiishi ni mtu mjini Mombasa ambaye alishtakiwa mahakamani na hivyo hatumjui mtu mwingine anayehusika,” alisema Bw. Kimaiyo said.

Mumewe wa kwanza, Jermaine Lindsay, alijilipua katika shambulizi la kujitoa mhanga nchini Uingereza mwaka 2005.

Alikuja Afrika mwaka 2009 na amekuwa akizunguka na kuishi barani huku kwa zaidi ya miaka 2.

Taarifa hizi zimeibuka wakati Wabunge wakiahidi kutumia mamlaka yao kuubadilisha kabisa mfumo wa usalama, ikiwa ni pamoja na kuzifunga kambi za wakimbizi na kuwaondoa wakuu wa usalama wenye utendaji mbovu.

Wakati kamati mbili za ulinzi na usalama zikianza kuwahoji wakuu wa usalama leo, waliahidi kwenda kwenye kiini cha shambulizi la Westgate, ikiwemo kuchungumza utendaji wa idara za usalama zinazochunguza tukio hilo katika wakati ambapo kuna madai ya wizi uliofanywa na wanausalama kwenye jingo hilo.

“Tunataka kujua ukweli kuhusu kilichotokea Westgate, ikiwa ni pamoja na kujua historia, wahusika na kilichosababisha kushindwa kulidhibiti tukio hilo,” alisema mwenye kiti wa kamati ya ulinzi na uhusiano wa kimataifa, Ndung’u Gethenji.

Wahid alikamatwa mwaka 2011 baada ya polisi kubaini kuwa nyumba yake ya mjini Mombasa ilikuwa imegeuzwa kuwa kiwanda cha kutengenezea mabomu kikiendeshwa na Lewthwaite na washirika. Hakupelekwa mahakamani.

Awali alikuwa akitambuliwa kama mtu aliyepangisha nyumba aliyokuwa akiishi Lewthwaite, lakini haikuwa ikifahamika wazi ni kwa kiasi gani alikuwa na taarifa za vitendo vya kigaidi vilivyokuwa vikifanywa na mkewe.

Lakini jana, Al-Shabaab ilisisitiza kuwa hakuna mwanamke aliyeshirikiana nao katika shambulio la Nairobi, na kukanusha taarifa kuwa “Mjane Mweupe’ alishiriki katika mauaji hayo.


“Kwa mara nyingine tunatangaza wazi kuwa hakuna mwanamke aliyehusika na tukio la Westgate,” walisema Al-Shabaab kwenye akaunti yao ya Twitter, wakisisitiza juu ya sera yao ya “kutowatumia wanawake katika operesheni kama hizo”.

Wakati huo huo, ripoti kutoka Somalia zinasema kuwa jana kiongozi mmoja wa dini ya Kiislamu katika mji wa Hargeisa alikamatwa kuhusiana na shambulizi la Westgate.

Mohamoud Abdullahi Ghelle alikamatwa kwa madai ya kuunga mkono shambulizi hilo lililogharimu maisha ya watu 67 na kuwajeruhi zaidi ya 175.

Inasemekana kuwa uhusiano wa Wahid na Lewthwaite “umewapa tabu wapelelezi, hasa ikizingatiwa kuwa aliwahi kuwa mwanajeshi na aliwahi kufanya kazi kama afisa usalama nchini Afghanistan, akiwalinda wamagharibi dhidi ya mashambulizi ya Wataleban”.


Mapema jana Jumatatu, Shirika la Msalaba mwekundu nchini Kenya lilitangaza kuwa idadi ya watu waliopotea baada ya shambulio la Westgate imeshuka mpaka 39 kutoka ile ya awali ya watu 60.

Katibu Mkuu wa shirika hilo, Abbas Gullet, alisema kuwa watu 14 kati ya wale waliokuwa wameripotiwa kupotea walikutwa wakiwa hai na kuruhusiwa kutoka hospitali mbalimbali, huku watu saba wakithibitika kufariki dunia.


CHANZO: DAILY NATION
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment