ASKOFU AJIUZULU KWA TUHUMA ZA KUMLINDA MHALIFU

File photo of Pope Francis


Papa Francis wa Kanisa Katoliki Duniani amekubali rasmi ombi la kujiuzulu kwa askofu mmoja wa Ireland aliyekiri kumlinda kasisi mmoja aliyetuhumiwa kwa udhalilishaji wa watoto.

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Vatican leo, William Lee, Askofu wa Dayosisi ya Waterford na Lismore za Ireland Kusini, aliondolewa kwenye majukumu yake hayo chini ya Sheria ya Kanisa inayohusisha makosa makubwa.

Mwaka 2010, Askofu Lee, aliyetawazwa mwaka 1966, alikiri kwamba majibu yake kuhusu tuhuma za udhalilishaji wa watoto zilizokuwa zikimkabili kasisi mmoja wa Ireland katikati ya miaka ya 1990 hazikuwa hayakuwa sahihi, na alifanya hivyo ili kumlinda mtuhumiwa.

Katika miaka ya hivi karibuni, Kanisa Katoliki limekuwa likilaumiwa kwamba linaficha maovu ya udhalilishaji wa watoto unaofanywa na makasisi ili kuwalinda na pia kulinda heshima ya kanisa.

Hivi karibuni mimia ya kesi yamefunguliwa huko Ulaya na Marekani zikiwahusisha watumishi hao.

Matukio ya udhalilishaji wa kingono ndani ya Kanisa Katoliki yaliibuka katika miaka ya 1980 na kugundulika mwaka 2002 baada ya mfumo wa kuyafunika kufichuliwa.


Haya yahatokea wakati Papa mpya akikabiliwa na mlima mkubwa wa tuhuma za udhalilishaji wa kingono zinazoliandama kanisa na kitisho cha usekula.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment