WAZIRI MKUU WA UTURUKI ALAANI SHAMBULIZI LA NAIROBI

Erdoğan slams terrorism in the name of Islam


WAZIRI Mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdoğan, amelaani vikali shambuli la kigaidi lililofanywa hivi karibuni na kundi la al-Shabaab lenye mafungamano na al-Qaeda kwenye kituo cha kibiashara mjini Nairobi, akisema kuwa Uislamu hauruhusu kuua raia wasiokuwa na hatia.

Akizungumza jana katika mkoa wa Denizli, magharibi mwa Uturuki, alisema: “Wanadai kuwa wanafanya hivi kwa jina la Uislamu. Sikilizeni: Mwenyezi Mungu hajampa mtu mamlaka ya kuwaua watu wasiokuwa na silaha wala ulinzi. Kumuua mtu mmoja ni sawa na kuwaua watu wote. Hivi ndivyo dini yetu inavyosema.”

Katika shambulizi la wiki iliyopita kwenye jengo la biashara la Westgate mwanamke mmoja wa Kituruki, Elif Yavuz, aliuawa. Mwanamke huyo kutoka Chuo Kikuu cha Harvard alikuwa akitarajia kujifungua ndani ya wiki mbili. Mume wake, mhandisi mwenye uraia wa Australia, Ross Langdon, naye pia aliuawa katika shambulizi hilo.



Aidha, Erdoğan alilaani vikali shambulizi lililofanywa wiki iliyopita kwenye kanisa moja mjini Peshawar, nchini Pakistan na kuua waumini 85.

“Tunalaani vitendo vyote vya kinyama vinavyofanywa Iraq, Yemen, Lebanon na Syria. Ugaidi hauna dini, na kamwe hatuwezi kukubali neno ‘Uislamu’ na ‘Ugaidi’ kuwekwa pamoja… Wale wanaojaribu kuyaweka pamoja maneno haya ili kutengeneza chuki dhidi ya Uislamu ni wabaguzi. Wale wanaotofautisha kati ya magaidi wazuri na magaidi wabaya ni wahalifu na ndio wanaolea ugaidi.”


Makundi ya Al-Shabaab na al-Qaeda yalitangaza kuungana mwezi Februari 2012. 


CHANZO: TodayZaman
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment