‘MJANE MWEUPE’ SAMANTHA HAJAFA





Vikosi vya Ulinzi vya Jeshi la Kenya (KDF) vimeiambia polisi ya Kimataifa (Interpol) kwamba hawakumuua mwanamke mwenye asili ya Uingereza anayedaiwa kuratibu shambulio kwenye kituo cha biashara cha Westgate jijini Nairobi.

Kwa mujibu wa taarifa mpya kutoka Shirika la Habari la Uingereza (BBC), Samantha Lewthwaite anayejulikana kama “mjane mweupe” anazunguka kwa uhuru katika mitaa ya Kenya na Interpol wametoa kibali cha kukamatwa.

Taarifa zinazopingana kutoka kwa Mamlaka za Kenya zinasema kuwa Samantha hakuwa miongoni mwa wavamizi waliouawa na KDF katika shambulizi la Jumatatu. Wavamizi watano waliuawa wakati wa mzingiro huo.

Samantha Lewthwaite, amewekwa katika orodha ya watu wanaosakwa sana na mamlaka za Kenya kwa kupanga shambulizi la kigaidi.

Samantha anadaiwa kuwa mtu hatari sana kwa mujibu wa shirika la ujasusi la Marekani (CIA) na lile la Israel (Mossad), na anahusika na vifo vya maafisa wa polisi katika jengo hilo; huko nyuma alifanikiwa kuikwepa mitego yote ya polisi ndani na nje ya Kenya.

Marekani imetoa kitita cha dola milioni 1 kama zawadi iwapo atakamatwa akiwa hai au maiti.


CHANZO: Kenyan Daily Post
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment