LIBYA YAANZA KUMEGUKA

 



MKOA wa kusini magharibi wa Fezzan nchini Libya jana ulijitangaza kuwa jimbo huru na lenye serikali.

Vyombo vya habari nchini Libya vimeripoti kuwa Nouri Mohammad al-Qouizi alitangazwa kuwa rais wa jimbo hilo. Viongozi wa kikabila katika eneo hilo wanasema kuwa baadaye watamteua mkuu wa jeshi atakayelinda mipaka ya jimbo hilo na mali asili zake.

Aidha, viongozi hao wa kikabila wanasema kuwa wamechukua hatua hiyo kwa sababu ya “utendaji dhaifu wa Baraza Kuu la Kitaifa na kutoitikiwa kwa matakwa ya watu wa Fezzan.”

Hatua hiyo inakuja mwezi mmoja baada ya eneo la Cyrenai, mashariki mwa Libya, kuchukua hatua kama hiyo kwa kujitangaza kuwa jimbo huru.

CHANZO: Al-Arabiya


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment