MUHTASARI WA HISTORIA YA MAJARIBIO YA NYUKLIA YA KOREA KASKAZINI

 News of North Korea's latest nuclear test came hours after state TV showed pictures of a new hydrogen bomb [Reuters]

Korea Kaskazini imefanya majaribio 6 ya silaha za nyuklia – likiwemo jaribio la Jumapili ya leo. Jaribio la kwanza lilitokea zaidi ya muongo mmoja uliopita katika harakati za taifa hilo kuwa miongoni mwa mataifa machache yanayomiliki silaha za nyuklia.

Oktoba 2006 - Pyongyang ilifanya jaribio lake la kwanza la silaha za nyuklia katika handaki moja katika eneo la Punggye-ri lenye milima mingi kaskazini mwa nchi hiyo.

Jaribio hilo lilisababisha mlipuko wa kilotani (kilotani moja = tani 1,000) hatua ambayo ililaaniwa na jumuiya ya kimataifa.

Baada ya jaribio hilo, Wakala wa Jiolojia nchini Marekani (USGS) ilisema kuwa ilibaini tetemeko la lenye uzito wa kiwango cha 4.2 kwenye Rasi ya Korea.

Mei 2009 - Pyongyang ilifanya jaribio lake la pili. Mlipuko wake, kama ilivyokuwa kwa jaribio la mwaka 2006, ulifanyika chini ya ardhi. Wakala wa Jiolojia nchini Marekani ilisema kuwa jaribio la bomu hilo lilisababisha tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 4.7 katika eneo la Kilju kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Mlipuko huo ulikuwa na uzito unaokadiriwa kuwa kilotani 2-8. Mlipuko huo ulisikika katika mji wa Yanji nchini China ambao uko mpakani kwenye umbali wa kilometa 200.

Februari 2013 – Nchi hiyo ilifanya jaribio la tatu na la kwanza chini ya utawala mpya wa Kim Jong-un. Jaribio hilo lilikuwa kubwa zaidi ya majaribio mawili ya mwanzo ambapo wataalamu walikadiria kuwa bomu hilo lilikuwa na uzito wa kilotani sita mpaka saba.


Pyongyang ilisema kuwa ilitumia “kifaa cha nyuklia kilichopunguzwa nguvu lakini chenye nguvu ya mlipuko mkubwa zaidi ya milipuko ya mwanzo”.

Wataalamu nchini Japan, Korea Kusini na Marekani walisema kuwa tetemeko katika eneo la Punggye-ri likuwa na nguvu kati ya 4.7 na 5.2.

Januari 2016 – Korea Kaskazini ilisema kuwa ilifanya jaribio la nne la bomu la hydrogen. Tetemeko la ukubwa wa 5.1 lilibainika takriban kilometa 50 kutoka mji wa Kilju, jirani na eneo la Punggye-ri ambalo kuna vinu vya nyuklia.

Wataalamu walikadiria kuwa bomu hilo lilikuwa na uzito wa kati ya kilotani nne na sita.

Septemba 2016 – Tetemeko lenye ukubwa wa 5.3 lilitokea baada ya mlipuko wa takribani kilotani 10 – mara 10 zaidi ya jaribio la kwanza lililofanywa na Pyongyang muongo mmoja uliopita.

Tetemeko hilo, kama lile la miezi tisa kabla, lilibainika karibu na eneo la majaribio ya nyuklia kwenye mahandaki ya Punggye-ri.

Septemba 2017 – Tetemeko la ukubwa wa 6.3 labainika katika eneo la Kilju, mahala linapopatikana eneo la majaribio ya nyuklia la Punggye-ri. Jaribio hilo jipya ndio jaribio kubwa kabisa kufanywa na Korea Kaskazini mpaka sasa.

Jaribio hilo ambalo ni la kwanza tangu Rais Donald Trump aingie madarakani, linakadiriwa kuwa na uzito wa mpaka kilotani 100 – karibu mara nne mpaka tano ya bomu ambalo Marekani ililidondosha kwenye mji wa Nagasaki nchini Japan.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment