MILIPUKO YAUTIKISA MJI MKUU WA INDONESIA


انفجارات وإطلاق نار قرب مكتب الأمم المتحدة في جاكرتا


Milipuko miwili ya mabomu imeutikisa mji mkuu wa Indonesia, Jakarta, huku ripoti zikisema kuwa kwa uchache watu wanne wamepoteza maisha.

"Watu wanne wamekufa, polisi mmoja na raia watatu,” shirika la habari la AFP limemnukuu msemaji wa polisi nchini humo, Anton Charliyan, akisema.

Kwa mujibu wa akaunti rasmi ya polisi kwenye mtandao wa Twitter, mlipuko mmoja umetokea karibu na eneo la biashara liitwalo Sarinah mall.

Ufyatuaji wa risasi ulisikika baada ya mlipuko wa asubuhi katika eneo hilo ambalo pia lina hoteli za kifahari, balozi na ofisi mbalimbali.

Charliyan amesema milio ya risasi imekoma lakini washambuliaji bado hawajakamatwa, na polisi wana wasiwasi kuwa kutakuwa na milio zaidi ya risasi.

Mashuhuda walionukuliwa na shirika la habari la Associated Press, wamesema kuwa mlipuko huo ulisababishwa na bomu, lakini hakukuwa na uthibitisho wa haraka wa madai hayo.

Kituo kimoja cha televisheni kutoka nchini humo kimesema kuwa jumla ya milipuko sita ilisikika.

Hakukuwa na maelezo ya haraka kuhusu wahusika wa mashambulizi hayo.

Indonesia imekuwa kwenye tahadhari kufuatia vitisho vya makundi ya wanamgambo huku polisi wakianzisha msako na operesheni dhidi ya watu wanaoshukiwa kuwa na mafungamano na makundi yenye siasa kali.

Wakati wa kilele cha Mwaka Mpya kiasi cha polisi na askari 150,000 walipelekwa kuimarisha ulinzi kwenye maeneo ya makanisa, viwanja vya ndege na maeneo mengine ya umma.


Pia zaidi ya polisi 9,000 walipelekwa mjini Bali, eneo ambalo lilitokea shambulizi baya la kigaini lililoua watu 202 mwaka 2002.











Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment