MATAIFA MENGI YAZIDI KUINGA MKONO SAUDIA ARABIA KATIKA MGOGORO WAKE NA IRAN


Moshi mkubwa ukionekana ndani ya jengo la ubalozi wa Saudi Arabia mjini Tehran baada ya waandamanaji wenye hasira kuuvamia mapema Jumapili. 

Qatar imekuwa nchi ya karibuni kabisa kuiunga mkono Saudi Arabia katika mgogoro wake na Iran, na kuchukua hatua za kumuita nyumbani balozi wake wa Tehran kama radiamali dhidi ya mashambulizi yaliyofanywa na waandamanaji dhidi ya ubalozi wa Saudia mjini Tehran wiki iliyopita.

Jordan, Djibouti, na Uturuki zimeelezea kuiunga mkono Saudi Arabia dhidi ya kitendo cha kushambuliwa ubalozi wake kufuatia kunyongwa kwa kiongozi maarifu wa kishia katika taifa hilo linaloongozwa na Wasunni.

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan amesema kuwa kunyongwa kwa watu 47 kwa makosa ya ugaidi nchini Saudi Arabia lilikuwa suala la “ndani”. Miongoni mwa walionyongwa ni sheikh wa kishia, Nimr al-Nimr – hatua iliyoibua ghadhabu za kimadhehebu katika ukanda huo.

"Watu arobaini na sita kati ya walionyongwa ni Wasunni na walinyongwa kwa sababu walikuwa na uhusiano na al-Qaeda. Mmoja wao alikuwa kiongozi wa kidini wa kishia. Uamuzi huu ulichukuliwa mapema na Saudi Arabia ikautekeleza. Huu ni uamuzi wao,” Erdogan alisema katika hotuba yake katika mji mkuu wa Uturuki, Ankara.

Aidha, Rais huyo alisema kuwa wale walionyamazia vifo vya watu katika vita vya Syria wanalalama kwa kunyongwa mtu mmoja nchini Saudi Arabia, akionekana kuisema Iran ingawa hakutaja majina.

"Mnaunga mkono [utawala wa Syria] kwa siri au kwa dhahiri. Mnatoa msaada wa kifedha na silaha kwa muuaji [Rais Bashar] Assad," Erdogan alisema. "Ubalozi wa Saudi Arabian embassy [nchini Iran] ulishambuliwa kwa mabomu. Ubalozi wake nchini Iraq pia ulihujumiwa. Hili jambo halikubaliki katika uhusiano wa kimataifa.”

Wakati huo huo, Rais wa Iran, Hassan Rouhani, aliitaka mahakama nchini humo kuwachukulia hatua haraka sana wale walioushambulia ubalozi wa Saudia.

"Kwa kuwaadhibu washambuliaji na wale waliochochea uhalifu huu wa wazi, tutapaswa kukomesha moja kwa moja hasara hiyo na matusi hayo dhidi ya heshima ya Iran na usalama wa taifa,” Rais Rouhani alinukuliwa akisema katika barua iliyochapishwa na shirika la habari nchini humo la IRNA.

Nayo Djibouti imekata uhusiano wake wa kidiplomasia na Iran katika kupinga kitendo cha kushambuliwa ubalozi wa Saudi Arabia. Nchi hiyo imeungana na Saudi Arabia, Bahrain na Sudan katika kukata kabisa uhusiano na Iran.

"Djibouti imekata uhusiano wake wa kidiplomasia na Iran katika kuonesha mshikamano na Saudi Arabia," Waziri wa Mambo ya Nje, Mahamoud Ali Youssouf, ameliambia shirika la habari la Reuters kwa ujumbe wa maandishi.

Qatar, Umoja wa Falme za Kiarabu na Kuwait zimewaita mabalozi wao walioko Iran.

Wakati huo huo, Jordan imemuita balozi wa Iran mjini Amman na kulaani shambulizi dhidi ya ubalozi huo, na “uingiliaji kati wa Iran” katika mambo ya Waarabu, shirika la habari la Jordan Petra, limesema.


Waandamanaji wa Kiiran waliuvamia ubalozi wa Saudia na majengo mengine ya kidiplomasia siku ya Jumapili. Tangu kutokea kwa mashambulizi hayo, Iran inasema kuwa imewakamata washambuliaji hao na kulaani ghasia hizo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment