NDEGE YAPOTEA IKIWA NA ABIRIA 54

A file photo of a Trigana Air ATR 42 turboprop

Ndege moja ya Indonesia iliyobeba abiria 54 imepoteza mawasiliano na chumba cha kuongozea ndege katika jimbo la Papua nchini Indonesia.

Kwa mujibu wa ripoti za awali, ndege hiyo ni ndege ya shirika la ndege la Trigana Air ATR 42, na imepoteza mawasiliano baada ya kuondoka katika uwanja wa ndege wa mji mkuu wa jimbo hilo, Jayapura na ilikuwa ikijiandaa kutua katika wilaya ya Oksibil yenye milima mingi.


Kwa mujibu wa mkurugenzi wa operesheni wa shirika hilo, Beni Sumaryanto, ndege hiyo iliwasiliana na chumba cha kuongozea ndege katika uwanja wa ndege wa Oksibil dakika kumi kabla ya kutua na kuomba kutua. Lakini, ndege hiyo haikuwasili.

Shirika la Trigana lilituma ndege nyingine kwenda kuitafuta, lakini nayo ililazimika kurudi kutoka na hali mbaya ya hewa katika eneo hilo ambalo linajulikana kuwa na hali ya hewa isiyotabirika.
Ndege hiyo ilikuwa imebeba watu wazima 44, watoto 5, na wafanyakazi 5.

Japokuwa wizara ya Uchukuzi ya Indonesia imesema kuwa sababu ya kutoweka kwa ndege hiyo haijulikani, Sumaryanto anasema kuwa hali mbaya ya hewa inaweza kuwa imechangia kupotea kwa ndege hiyo.

Wiki iliyopita, ndege moja ya shirika la ndege la Komala Air la nchini Indonesia, ilipata ajali katika wilaya ya Yahukimo katika jimbo la Papua, iliyosababisha kifo cha mtu mmoja na wengine watano kujeruhiwa vibaya sana. Ajali hiyo ilisemekana kusababishwa na hali mbaya ya hewa.

Katika miezi ya hivi karibuni, Indonesia imekumbwa na jinamizi la usalama mdogo wa usafiri wake wa anga.


Mwezi Desemba mwaka jana, ndege ya shirika la ndege la  AirAsia iliyokuwa ikisafiri kutoka mji wa Surabaya nchini humo kwenye Singapore ilipata ajali katika Bahari ya Java kutokana na hali mbaya ya hewa na kusababisha vifo vya watu wote 162 waliokuwa ndani ya ndege hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment