MILIPUKO MIWILI YAUA ZAIDI YA WATU 13 NCHINI NIGERIA


The scene of a bombing where at least 20 people were killed in Maiduguri, northeast Nigeria, June 22, 2015 (AFP photo)
Eneo la mlipuko lililoua watu wasiopungua 20 katika mji wa Maiduguri, kaskazini mashariki mwa Nigeria, Juni 22, 2015.


Milipuko miwili ya mabomu katika eneo la soko na kizuizi cha jeshi katika eneo la kaskazini mashariki ya Nigeria imewaua watu kadhaa.

Mlipuko wa kwanza umetokea katika soko lenye msongamano katika kijiji cha Malari, nje ya mji wa Maiduguri. Kwa uchache watu 10 wamepoteza maisha katika mlipuko huo.

Dakika kadhaa baadaye, gari aina ya taksi lililipulika katika kizuizi kimoja cha jeshi na kuwaua abiria wawili na afisa usalama mmoja.
Mpaka sasa hakuna kundi lililodai kuhusika na mashambulizi hayo huku ghasia zikigharimu maisha ya zaidi ya watu 160 ndani ya wiki moja nchini humo.

Lango kuu la soko mjini Maiduguri lililofungwa Machi 7, 2015 baada ya mlipuko wa bomu.

Katika mashambulizi hayo mabaya, wanamgambo wanadaima kuilenga misikiti kadha katika mji wa kaskazini mashariki wa Kukawa mnamo Juni 30 na kuwaua waumini wapatao 100.

Wanamgambo hao wameongeza mashambulizi yao tangu Rais Muhammadu Buhari alipoingia madarakani mwishoni mwa mwezi Mei.

Rais Buhari, ambaye ni jenerali mstaafu, ameapa kupambana na kundi la Boko Haram na kuliteketeza kabisa.


Uasi wa kundi hilo ulianza mwaka 2009 na umesababisha vifo vya watu wapatao 15,000 ndani ya miaka sita.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment