RAIS KIKWETE AMTUMA MJUMBE MAALUMU KWENDA RWANDA





Rais Jakaya Kikwete amemtuma msaidizi wake maalumu, Profesa Mark Mwandosya, kwenda Kigali katika wakati ambapo uhusiano wa kidplomasia baina ya nchi hizi mbili umekuwa ukiyumbayumba.


Taarifa ya Ikulu imesema kuwa Prof Mwandosya, ambaye ni Waziri wa nchi katika ofisi ya Rais, asiyekuwa na wizara maalumu, aliondoka siku ya Jumamosi na atakuwa nchini Rwanda kwa zaira ya rasmi itakayodumu kwa muda wa wiki nzima ‘kuona jinsi Rwanda inavyopanga na kutekeleza huduma za kijamii na kiuchumi’.

Tanzania na Rwanda zimekuwa katika uhusiano usioridhisha kutoka na ushauri uliotolewa na Rais Kikwete mwezi Mei mwaka jana kuwa Rwanda ifanye mazungumzo na waasi wa FDLR kama sehemu ya juhudi za kukomesha mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Rwanda ilikasirishwa na ushauri huo na kusema moja kwa moja kuwa hawawezi kukaa meza moja na wauaji. Marais wa nchi hizi mbili – Kikwete na Kagame- walikutana mwezi Agosti mwaka jana mjini Kampala na kufanya mazungumzo juu ya suala hilo.


CHANZO: the Citizen
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment