BUNGE MAALUMU LAANZA RASMI VIKAO VYAKE


Bunge maalum la katiba limemchagua Mh. Pandu Ameir Kificho kuwa mwenyekiti wa muda wa bunge hilo huku baadhi ya wajumbe wakilalamikia kitendo walichokiita ujanja wa serikali wa kuchelewesha kwa makusudi nakala za kanuni za kuendesha bunge la katiba kwa madai ya kuwanyima fursa wajumbe hao kuzipitia kikamilifu ili kuepusha malalamiko na hatimae kupata katiba iliyo bora kwa manufaa ya Watanzania

Mwenyekiti huyo wa muda ambaye ni Pandu Ameir Kificho amepatikana kutokana na nafasi hiyo kuombwa na wajumbe wanne ambao ni Mh Pandu Amri Kificho,Magdalena Rubangula na Prof Costa Ricky Mahalu na kupata fursa ya kujieleza na kuulizwa maswali kadhaa na wajumbe na baadae wajumbe hao kupata fursa ya kupiga kura ya kumchagua mwenyekiti huyo aliyetangzawa na katibu wa bunge.

Awali kabla ya kuanza kwa zoezi  la kupiga kura ya mwenyekiti wa muda katibu wa baraza la wawakilishi Zanzibar  Yahaya Hamis Hamad alisoma tangazo la rais la kuitisha  bunge maalum la katiba kuashirika kwamba vikao vya bunge hilo vimeanza rasmi.

Mapema asubuhi  wajumbe hao wa bunge maalum la katiba wamepata maelekezo ya ukaaji na jiografia ya ukumbi na baadae kupata fursa kuuliza maswali na kutoa michango mbalimbali ambapo baadhi ya wabunge wametaka uwepo wa usawa wa jinsia katika uongozi wa bunge hilo na wengine kutaka kupata kanuni za kuendesha bunge hilo ili waweze kutoa michango iliyo bora.


Nje ya ukumbi wa bunge tofauti na mabunge mengine katika bunge hili maalumu  la katiba ulinzi uliimarishwa maradufu ambapo vikosi vya polisi wa doria pamoja na vikosi vya mbwa na farasi vilikuwa vikirandaranda katika kila kona ya eneo la ndani na nje ya uzio wa bunge
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment