BINTI WA KIMSRI AJIPIGA RISASI BAADA YA KUKATAA KUVAA HIJAB


Binti mmoja wa Kimisri mwenye umri wa miaka 15 aliyekataa shinikizo la familia yake kumtaka avae vazi la Kiislamu, yaani hijabu, alijipiga risasi kwa kutumia bastola ya baba yake, tukio hilo limeripotiwa na vyombo vya habari vya Misri na eneo zima la Mashariki ya Kati.

Tukio hilo la kujiua, lililotokea wiki iliyopita huko katika wilaya ya Giza, liliripotiwa na tovuti maarufu ya habari nchini humo ijulikanayo kama  Youm7.

Binti huyo aliyetambulika kwa jina la Amira, anaelezewa kupata msukosuko kutoka kwa familia yake baada ya kuondosha hijabu yake.

Kwa mujibu wa tovuti hiyo, uchunguzi uliofanywa ulibaini kuwa kutokana na hali hiyo, Amira aliamua kuingia ndani na kuchukua silaha ya baba yake na kujiua.

CHANZO: al Arabiya
Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment