WIZKID ANAKABILIWA NA KIFUNGO CHA MIAKA 11 JELA

wizkid1

Mahakama nchini Uganda imetoa kibali cha kukamatwa kwa mwanamuziki maarufu wa Nigeria, Wizkid, kwa kushindwa kutoa kwenye onesho la burudani.

Kibalo hicho kinamtaka afisa yeyote wa polisi kutoka Uganda au polisi ya Kimataifa (Interpol) kumkamata Wizkid na kumfikisha mahakamani kabla ya tarehe 16 Januari mwaka 2017.

Waganda walisikitishwa na kitendo cha mwanamuziki huyo kutooneka kwenye onesho la muziki lililopangwa kufanyika tarehe 3 Desemba katika Uwanja wa Cricket wa Lugogo mjini Kampala.

Kibali hicho kimetolewa kwa msingi kwamba muimbaji huyo alijipatia pesa kwa njia ya hila, udanganyifu na kufanya hujuma. Mbali na mashitaka hayo, waandaaji wa tamasha hilo, Face TV na wanasheria wanataka ahukumiwe kifungo cha miaka 11 jela iwapo hatarejesha fedha alizolipwa.

Licha ya kuwasababishia hasara ya tiketi za kiingilio na tiketi ya ndege, gharama za hoteli, eneo na matangazo ambayo yaligharimu zaidi ya dola 300,000, waandaaji wa onesho hilo pia walimlipa meneja wa Wizkid dola 60,000 kama malipo yake ya kutumbuiza, dola 5000 ya udalali na dola 3000 za matumizi kwa siku zote ambazo mwanamuzi huyo na timu yake wangekaa nchini humo. Aidha, zaidi ya watu 25,000 walikuwa wamenunua tiketi ili kushuhudia onesho hilo.

Kwa mujibu wa mtandao wa Mediamax, hivi karibuni Wizkid alikuwa nchini Marekani kwa sababu za kimatibabu na kwa mujibu wa waandaaji, Wizkid hakuweza kupanda ndege kutoka Marekani mpaka Uganda kutokana na “mazingira yasiyoepukika”.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment