RAIS WA GAMBIA AYAKATAA MATOKEO YA UCHAGUZI WIKI MOJA BAADA YA KUKUBALI KUSHINDWA

An image grab from Gambian state television broadcast on December 2, 2016 showing Gambian President Yahya Jammeh speaking after being defeated during the presidential election. (Photo by AFP)
Picha kutoka televisheni ya serikali iliyopigwa Desemba 2, 2016 ikimuonesha Rais wa Gambia Yahya Jammeh akizungumza baada ya kushindwa katika uchaguzi wa urais. 


Rais wa Gambia Yahya Jammeh ameyakataa matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika hivi karibuni nchini humo wiki moja baada ya kukubali kushindwa na mpinzani wake.

"Hivyo basi ninatangaza kuyakataa matokeo yote," Jammeh alisema katika taarifa iliyorushwa kwenye kituo cha televisheni cha serikali usiku wa kuamkia leo, akisisitiza kuwa uchunguzi uliofanywa tangu Desemba mosi umeonesha kuwa kulikowa na ukiukaji wa taratibu katika uchaguzi huo, jambo ambalo amesema kuwa halikubaliki.

"Ninarudia: Sitayakubali matokeo kutokana na kilichotokea," aliongeza Jammeh ambaye ameitawala nchini hiyo ya Afrika Magharibi kwa zaidi ya miaka 22.

Wakati wa taarifahiyo, kiongozi huyo alieleza kuwa baadhi ya taarifa katika matokeo ya uchaguzi zilifanyiwa hila na kwamba wapiga kura walinyimwa haki ya kupiga kura.

"Uchunguzi wetu umebaini kuwa katika baadhi ya matukio wapiga kura waliambiwa kwamba tayari upinzani ulikuwa umeshinda na hivyo hawana haja ya kupiga kura, hivyo baadhi yao kwa hasira wakarudi nyumbani," Jammeh alisema.

Wafuasi wa upinzani wakishangilia baada ya kiongozi wao  Ousainou Darboe pamoja na wapinzani wengine 18 kuachiwa huru kwa dhamana mnamo Desemba 5, 2016 mjini Banjul, siku chache tu baada ya upinzani kushinda uchaguzi.

Kauli hiyo inakuja ikiwa imepita wiki moja tu tangu alipoonekana katika televisheni ya serikali akimpigia mgombea wa upinzani Adama Barrow na kumtakia kila la heri huku akionekana kuwa mwenye furaha.

"Wewe ni rais mteule wa Gambia, nami ninakutakia kila la heri," Jammeh alimwambia Barrow siku hiyo na kuongeza kuwa hana kinyongo naye.


Uamuzi huo wa kurudi nyuma unatarajiwa kuibua ghadhabu na hasira miongoni mwa wapinzani na idadi kubwa ya Wagambia wanaoishi uhamishoni katika mataifa ya nje.

Hayo yanatokea wakati ambapo wiki moja tu baada ya Jammeh kukubali kushindwa, makumi ya wafungwa wa kisiasa wameachiwa huru kwa dhamana.

Kinachosubiriwa ni kuona iwapo taifa hilo la Afrika Magharibi lenye raia milioni 1.9 litavumilia kumuona Jammeh akiendelea kutawala.

Kufuatia matokeo ya uchaguzi wa wiki iliyopita, Wagambia walimiminika barabarani wakiimba na kucheza huku wakipiga nara za “Uhuru!”

Serikali za mataifa ya magharibi zimekuwa zikiukosoa vikali utawala wa Jammeh, hasa uamuzi wake wa kujiondoa kwenye umoja wa Jumuiya ya Madola ambao unazihusisha nchi zilizowahi kutawaliwa na Uingereza na uamuzi wake wa kujiondoa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Wakati akitangaza nchi yake kujiondoa katika Jumuiya ya Madola mwaka 2013, Jammeh aliielezea jumuiya hiyo kama “taasisi ya ukoloni mambo leo.” Pia mwezi Oktoba alitangaza kuwa Gambia itajiondoa ICC akiituhumu kuwa ni “Mahakama ya Kimataifa ya Ubaguzi.”


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment