MWANAMKE AHUKUMIWA NA MAHAKAMA KWA KUMTELEKEZA MUMEWAKE.

Roseline anadaiwa kuwatelekeza watoto wake wanaoishi na baba yao
Mwanamke mmoja nchini Kenya ameamrishwa na mahakama kumlipa mumewe shilingi elfu tatu au dola 35 kama hela za kukidhi mahitaji yake na watoto wake kila mwezi.

Mwanamke huyo kwa jina Roselyn Muyonga, ambaye anatuhumiwa kwa kuwatelekeza mumewe na watoto wake watatu , huenda akafungwa miezi mitano jela au kutozwa faini ya shilingi laki mbili ikiwa atakosa kutekeleza amri ya mahakama.
Mwanamume huyo hufanya kazi za kibarua.
Afisaa mmoja wa watoto katika jimbo la Kakamega Magharibi mwa Kenya, alisema kuwa mwanamke huyo alipuuza jukumu lake la kulea watoto wake baada ya yeye na mumewe kutalakiana.
Afisa huyo alisema kuwa wanaume huachiwa majukumu mengi sana wakati wanapoachwa na watoto na kwamba wanawake kama Roselyn wanapaswa kuamrishwa kuwatunza watoto wao hata kama wameachana na waume zao.
Tayari mashirika kadhaa yanataka kushinikiza sheria ya kuwashurutisha wanawake kutoa mchango kwa kuwalea watoto wao wanapoachana na mwanamume au baba ya watoto.
Kwa mujibu wa afisaa mmoja wa watoto, visa vya wanawake kuwatelekeza watoto wao katika jimbo hilo vimeongezeka.
Share on Google Plus

About www.habarika24.blogspots.com

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment